Thursday, June 12, 2014

FRANK KIWELE AWASHUKURU WALIOMCHANGIA

 

MMILIKI WA MTANDAO HUU KATIKATI  KULIA GEOFREY NYANG'ORO KATIKATI AKIMKABIDHI FEDHA ZA MSAADA FRANK KIWELE (21) FEDHA HIZO ZIMETOLEWA NA WASOMJA WA GAZETI LA MWANANCHI NA MCHANGO HUU NI KWAAJILI YA KUCHANGIA  GHARAMA ZA MATIBABU YA TATIZO LINALOMSUMBUA  TANGU KUZALIWA KWAKE

 WANAOSHUHUDI TUKIO HILO  KUSHOTO NA AFISA USTAWI WA JAMII MKUU WA MANISPAA YA IRINGA GASPER NSANYE NA KULIA NI MJOMBO WA KIJANA HUYO THOMAS NGANDANGO

 


 

HABARI



Iringa.Kijana Frenk Kiwele anayekabiliwa na tatizo la kutokwa na haja kubwa na ndogo mfulilizo amepkea msaada wa Sh 510,000 kutoka kwa wasomaji wa gazeti la Mwananchi na kudai sasa anapata matumaini ya kupona tatizo lake.

Kiwele alikabidhiwa fedha hizo juzi na mwandishi wa gazeti la Mwananchi  mkoani hapa  Geofrey Nyang’oro ambaye pia ndiye mmiliki wa mtandao huu,hafla hiyon amefanyika nyumbani kwake Kinegamgosi A  kata ya Ruaha ndani ya Mansipaa ya Iringa.

Hafla hiyo imeshuhudiwa na  Afisa Ustawi wa Jamii Mkuu wa Manispaa ya Iringa Gasper Nsanye na Mjomba wa kijana huyo Thomas Ngandango.

Akizungumza muda mufi baada ya kukabidhiwa fedha hizo  Frank aliwashukuru wasomaji wa Gazeti hilo  kwa kumchangia kiasi hicho cha fedha baada ya kusoma makala hiyo licha ya kuwa hawamjui na kudai mungu atawazidisha pale walipopungukiwa.

 Kwa mjibu wa taarifa ya madakati Bingwa kutoka Hosptali ya Taifa ya Muhimbili waliofanya uchunguzi wa tatizo lake wanadai gharama zinazohitajika kwa ajili ya matibabu ya Farnk Kiwele ni  Sh 3,650,750

Kwa upande wake Afisa Usitawi wa Jamii Mkuu wa Manispaa ya Iringa Gasper Nsanye amemshukuru mwandishi wa makala hayo, kampuni ya Mwananchi Communicationi LTD ambao ni wachapishaji wa magazeti ya Mwananchi,Thecitizen na Mwanaspoti kwa kukubali  kuchapisha makala hayao gazeti jambo liliwafanya wasomaji wake kuoisoma na kutoa kiasi hicho cha fedha.

 “Mini nianze kwa kumshukuru mwandishi wa makala haya,nilishukuru kampuni ya Mwananchi Communication LTD na pia wasomaji wa gazeti la Mwananchi kwa mchango wao,ofisi yetu inashughulikia suala hilo kw akaribu na hivi sasa tumefungua kitabu cha Benki katikA Benki ya NMB chenye akaunti namba ya FRANK ELIUTA KIWELE  A/C NO 16110000481”alisema Nsanye na kuongeza:

“Katika A/C hiyo kwenye kikao cha wakuu wa Idara na waheshimiw amadiwani wa Manispaa ya Iringa walichangia Sh 150,000 huku wadau wengine wa mkoani hapa wakitoa mchangia wa Sh 50 000 na kufanya jumla ya Sh 200,000 na kwa sasa tukichanganya na hizo tutakuwa na Sh 700,000”alisema Nsanye.

Nsanye alisema bado michango inahitajika kufikia kiwango kinachohitajika na kuongeza kuwa hata uongozi wa Manispaa hiyo unaendelea na mchakato wa kuwafikia wadau mbalimbali kwa ajili ya kufanikisha jukumu hilo.

Naye Mjumba wa Frank Thomas alitoa shukurani zake kwa makundi yote yalitoa mchango huo na kudai pindi kiasi hicho kitakapopatikana atakuwa bega kwa bega katika kuuguza mpya wake kazi aliyoifanya kw amda mrefu sasa.


MWISHO
 


Sunday, May 25, 2014

Kiwele:NAHITAJI SH 3.6 MILIONI KUPATA TIBA YA TATIZO LINALONISIBU

                        MAKALA
Ukikutana naye mitaani ama nyumbani kwake akiwa amepumzika na hata kama utamkuta akifanya baadhi ya shughuli kwa lengo la kujipatia kipato kamwe huwezi kuadhani kama kijana huyo  Frank Kiwele (21) anatatizo lolote.
Nikijana mtulivu na mwenye sura ya ucheshi mda wote utakapokuwa amekaa naye na hata kuzungumza na,ni vigumu kuamini kama anakabiriwa na tattizo la kutwa na haja kubw ana ndogo  tatizo lililodumu tangu kuzaliwa kwake hadi sasa.
“Tatizo hili nimezaliwa nalo kwani katika sehemu ya kiuono unapoanzia uti wa mgongo ninauvimbe,wataalamu wanasema ndio unaosababisha uwepo wa tatizo hilo,kimsingi limenitesa sana limenitenga na jamii na marafiki kutokana na kutokwa na haja ndogo na kubwa  bila mufulililozo bila ya hata kujitambua.”anasema Kiwele.
Kiwele ni mtoto wa pili katika familia ya Eliuta Kiwele ambaye amefariki duniani miaka 7 (mwaka 2007 akitanguliwa na mama mazazi wa Frank ,Sarah Ngadango aliyefariki mwaka 2002.

Kwa kifupi kiwele anasumbuliwa na tatizo la viongu vinavyotumika kuzuia haja ndogo na kubwa kutoka kushindwa kufanya kazi.

Binafsi ninatoa shukurani zangu za dhati  kwa wale waliofanikiwa kuyasoma makala ya Frenk Kiwele (21)katika gazeti la Mwananchi Mwananchi Jumapili toleo la Mei 3 mwaka huu.

Wengi wamehamsika na kuanza kumchangia mungua awabariki sana na awazidishie pale palipopungua ombi langu naomba muendelea kumchangii ili pamoja tuweze kumrejeshea kijana huyu matumaini ya kufurahia maisha yake hapa duniani.

CHAI BORA MUFINDI INAVYONOGESHA KOMBE LA "MUUNGANO MUFINDI CUP"

 Mwakilishi wa timu ya Zamalek ya Njombe kulia Shukuru Millinga akionyesha moja ya jezi alizokabidhiwa na Mkuu wa kitengo cha Uzalishaji cha Kampuni ya Chai Bora ya Mufindi Mkoani Iringa Petronilla Alphone kushoto kwenye wakati wa hafla ya kukabidhi vifaa hivyo iliyofanyika kwenye viwanja vya Kiwanda cha Chai bora  Mjini Mafinga Wilayani Mufindi mkoani Iringa,katikati ni mratibu wa michuoano hiyo Daud Yasini
Viongozi wa kiwanda cha Chai bora,chama cha Mpira wa miguu Wilaya ya Mufindi,waratibu kombe la Muungano na wawakilishi wa timu washiriki wa kombe la muungano wakiwa katika picha ya pamoja katika hafla ya kukabidhi vifaa vya michezo iliyofanyika kwenye viwanja vya kiwanda hicho mjini Mafinga mkoani Iringa,waliosimama ni wawakilishi watimu washiriki.




                                                           HABARi
KOMBE la Muungano “Muungano Cup” ambalo limeanza kutimua vumbi katika Viwanja vya  Igowole  na kile cha Wambi katika Wilaya ya Mufindi mkoani Iringa limepigwa jeki na kampuni ya  Chai Bora, kwa kupatiwa msaada wa jezi seti 6 pamoja na mipira 10 kwa ajili ya kuboresha mashindano hayo.
Akikabidhi jezi na mipira hiyo kwa mratibu wa mashindano hayo ya kombe la Muungano- Daud Yasin, mkuu wa idara ya uzalishaji wa Kampuni ya Chai Bora Petronilla Alphonce, alisema  lengo la msaada huo ni kuyafanya mashindano hayo kuwa na muonekano wa pekee, shughuli iliyofanyika katika uwanja wa Chai Bora mjini Mafinga,.
Petronida amesema vijana hao wanapaswa kujituma katika michezo ili kuonyesha vipaji  na uwezo nyanda za juu kusini, ikiwa pamoja na kutotumia vinywaji vyenye kileo ili kuwafanya wawe na nguvu imara.
Aidha amesema misaada hiyo imegharimu jumla ya shilingi Milioni 7.7  na kuwa kampuni kwa kutambua hilo imetoa msaada huo kwa wachezaji wote, na mchango huo ni katika kuunga mkono mashindano hayo kwa kuiwakirisha kampuni kwa kiwango cha hali ya juu.
“Kampuni kwa kuthamini michezo imeona ni vema itoe jezi seti 6 na Mipira kumi, vifaa vyenye thamani ya shilingi Milioni 7.7,  mchango huu tulioutoa tunajua una manufaa na utatuletea ushindani  mkubwa”alisema Petronilla
Akipokea msaada huo mratibu wa mashindano hayo ya Kombe la Muungano Daud Yasin alisema  kampuni ya Chai imekuwa kiyadhamini mashindano hayo tangu yalipoanzishwa mwaka  1998.
Amewataka wachezaji kuthamini vifaa hivyo kwa ubora wake kwani vina ubora wa hali ya juu, na kuwa matumaini yake ni vilabu shiriki kufanya vyema ili kuitangaza kampuni hiyo kupitia michuano hiyo inayozishirikisha timu za mikoa ya nyanda za juu kusini.
Alisema  mashindano hayo ambayo yamezinduliwa Mei 24 katika uwanja wa shule ya msingi Igowole ambapo mashindano hayo yataendeshwa katika viwanja viwili,  kwa maana ya kiwanja cha wambi cha mjini Mafinga na kiwanja Igowole shule ya msingi,
Uwanja wa Igowole utachezewa na timu ya Mbeya city ya jijini Mbeya, Zamalek na timu ya Igowole   sekondari,  huku mjini Mafinga katika uwanja wa Wambi kutakuwa na mechi ya timu ya Benk ya wananchi Mucoba, timu ya chuo cha Incoment na timu ya Black Cheeter ya mjini Iringa.
Amesema timu ya Mbaspo ambayo ni mabingwa watetezi waliochukua kombe la Muungano mwaka 2013 wamepewa fulsa ya kuingia moja kwa moja katika hatua ya nusu fainali, ambapo amewataka wapenzi wa soka na mashabiki kujitokeza kwa wingi kuangalia vipaji vya vijana wa nyanda za juu kusini.
Hata hivyo alisema mashindano hayo yamekuwa na msisimko kwa kuwa yanahusisha vijana walio na umri chini ya miaka 20, huku akiwataka wapenzi na mashabiki wa nyanda za juu kusini, kujitokeza kwa wingi kutazama vipaji vya vijana wa nyanda za juu kusini.
Daud Yasini alisema kwa mwaka huu  niwa mwisho kwake kuratibu mashindano ya kombe la Muungano kwani anastaafu na kuwa bingwa atachukua Kombe hilo moja kwa moja, kama ni kumbukumbu kwa timu ya uratibu wake wa mashindano hayo.
Yasini alisema  mashindano hayo yatakamilika  Juni 11 mwaka huu ambapo fainali ya kombe hilo mchezo wake utakachezwa katika uwanja wa Wambi wa mjini Mafinga.
MWISHO

MICHUANO KOMBE LA MUUNGANO MUFINDI

Mkuu wa kitengo cha uzalishaji wa kampuni ya Chai bora ya Mufindi makoani Iringa Petronilla Alphoce akipena mkono na

Lambardo Mvanda, mwakirishi wa timu ya Black Cheeter ya Iringa mjini  wakati wa hafla fupi ya kukabidhi msada wa vifaa vya michezo wenye thamani ya Sh 7.7 milioni,Katikati mratibu wa mashindano hayo Daud Yasini 

 


Saturday, May 24, 2014

Lumiye: Tumeanzisha chama kupinga manyanyaso



Mwenyekiti wa chama cha wafugaji Tanzania (CCWT) Ally Lumiye akizunguzunguza na wafugaji kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika kijiji cha mtakuja wilayani chunya jijini mbeya




                                                           HABARI

WAFUGAJI  kote nchini wameshauriwa kujiunga na Chama cha wafugaji Tanzania (CCWT) ili kuweza kukabiliana na changamoto mbalimbali zinazowakabili ikiwamo vitendo vya unyanyasaji walivyodai wamekuwa wakitendewa na baadhi ya  viongozi na watendahi serikalini.

Kauli hiyo imetolewa na Mwenyekiti wa (CCWT) Taifa Ally Lumiye alipokuwa akizungumza na wafugaji kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika kijiji cha Mtakuja wilayani Chunya Jijini Mbeya .

Ally amesema  kwa muda mrefu jamii ya wafugaji imekuwa ikitendewa vitendo vya kinyama ikiwamo kuhamishwa katika maeneo yao bila ya kufuata taratibu na wakati mwingine mifugo kukamatwa huku wafugaji wakitozwa ushuru mkubwa kitendo kinachochangia kuwafilisi.

Amesema  ndani ya chama hicho wafugaji watapata fursa ya kutetewa pindi wanapofanyiwa vitendo vya uonevu kwakuwa kimeajiri wanasheria kwa ajili ya kazi hiyo.

“Chama chetu kimepata usajil Desemba mwaka jana,kama mnavyofahamu jamii ya wafugaji imekuwa kitendewa vitendo vya unyanyasaji ,wafugaji kuhamishwa bila kufuata utaratibu,mifugo kukamatwa na kuzwa faini  kubwa na hata wakati mwingine kutaifishwa…sasa wafugaji mmepata mtetezi wenu mtumieni”alisema  Lumiye na kuongeza  kuongeza:

“Kwa sasa chama chetu kimeajili wanasheria ambao  jukumu lao ni kukusanya taarifa mbalimbali kutoka kwa wafugaji ili kuona kama kunawafugaji wametendewa vitendo vya ukiukwaji wa sheria hatua ziweze kuchukuliwa dhida ya wahusika”alisema.

Thursday, June 13, 2013

Watuta wafa kwa matukio tofauti Iringa


WATU  watatu waemefariki dunia katika matukio tofauti likiwamo tukio la mtu anaejulikana kwa jina la Roza Mazengo alifariki dunia alipokuwa akiogelea katika bwawa la Mtera .

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Iringa Ramadhani Mungi alisema kuwa tukio hilo lilitokea juzi majira ya saa tisa alasiri  maeneo ya kambi ya uvuvi Changarawe katika bwawa la Mtera.

Kamanda alisema kuwa chanzo cha tukio hilo ni ni baada ya kuzidiwa na maji wakati akiogelea na tukio hilo lilitokea katika kijiji cha Mgori kata ya Migori  wilaya ya Iringa vijijini.

Tukio lingine  lilitokea katika kijiji cha Lulaka wilaya ya Kilolo mtu aliye julikana kwa jina la Kwinindo Mwalusamba mwenye umri wa miaka 19  mkazi wa kijiji cha Lukani alifariki dunia  kuangukiwana mti aliokuwa akiukata kwa ajiri ya nguzo ya umeme.

Tukio hilo lilitokea juzi majira ya saa saba katika hospital ya wilay wakati akiendelea na matibabu,

Wakati huo huo katika maeneo ya Iguruba  kitongoji cha boma la ng’ombe tarafa ya Isimani Wilaya ya iringa vijijini mtu anayafahamika kwa jina la Majaliwa Bosco  alifariki dunia mara baada ya kung’atwa na nyuki alipokuwa anawarushia mawe juu ya mti chanzo kikiwa ni mchezo wa kitoto.

Lipuli yafufuka sasa kushiriki daraja la kwanza ngazi ya taifa msimu ujao

Timu ya Mpira wa Miguu ya Mkoani Iringa Lipuli inatarajia kurudi tena katika ulimwengu wa soka baada ya kufanikiwa kununua nafasi ya daraja la kwanza Tanzania bara iliyokuwa ikishikiliwa na timu ya Polisi mkoani hapa.

Taratibu za kununua time zimekamilika leo wakati Mdhamini Mkuu wa Timu hiyo Jesca Msambatavangu alipokabidhi Sh 14.5 milioni kwa ajili ya kuwasilisha malipo ya awali ya ununuzi wa timu hiyo.
Hatua hiyo imekuja kufuatia  Chama cha Mpira wa miguu Mkoa wa Iringa (IREFA)kutangza zabuni ya kuuzw akwa timu hiyo ambayo gharama za jumula zilikuwa Sh 20.5milioni.

Akizungumza muda mfupi baada ya kukabidhi hundi ya kiasi hicho cha fedha katika hafla iliyofanyika  leo asubuhi Rais wa timu Jesca alisema lengo la mkakati huo ni kukuza mchezi wa mpira wa miguu mkoani hapa.

Alisema baada ya kukamilika kwamchakato wa kwanza kazi itakayofuata ni kupanga safi ya uongozi,kuajiri kocha bora na kusajili kikosi kitachaosaidia kuipandishi timu hiyo ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara katika msimo ujao wa ligi.

Awali mwenyekiti wa Timu hiyo Abuu Changawa aliuelezea mafanikia ya mchakato huo kuwa ni sehemu muhimu katika kufanyamapinduzi ya soka mkoani hapa.

"Kwa muda mrefu tumekuwa tuhakihangaika kutaka kupandisha timu bila mafanikio,lakini hatua ya leo ni nzuri na nisema tumefurahi kuipata nafasi hii na tutahakikisha tunafanikiwa kufikia Ligi Kuu ya Vodacom msimo ujao"alisema Changawa