Thursday, June 13, 2013

Watuta wafa kwa matukio tofauti Iringa


WATU  watatu waemefariki dunia katika matukio tofauti likiwamo tukio la mtu anaejulikana kwa jina la Roza Mazengo alifariki dunia alipokuwa akiogelea katika bwawa la Mtera .

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Iringa Ramadhani Mungi alisema kuwa tukio hilo lilitokea juzi majira ya saa tisa alasiri  maeneo ya kambi ya uvuvi Changarawe katika bwawa la Mtera.

Kamanda alisema kuwa chanzo cha tukio hilo ni ni baada ya kuzidiwa na maji wakati akiogelea na tukio hilo lilitokea katika kijiji cha Mgori kata ya Migori  wilaya ya Iringa vijijini.

Tukio lingine  lilitokea katika kijiji cha Lulaka wilaya ya Kilolo mtu aliye julikana kwa jina la Kwinindo Mwalusamba mwenye umri wa miaka 19  mkazi wa kijiji cha Lukani alifariki dunia  kuangukiwana mti aliokuwa akiukata kwa ajiri ya nguzo ya umeme.

Tukio hilo lilitokea juzi majira ya saa saba katika hospital ya wilay wakati akiendelea na matibabu,

Wakati huo huo katika maeneo ya Iguruba  kitongoji cha boma la ng’ombe tarafa ya Isimani Wilaya ya iringa vijijini mtu anayafahamika kwa jina la Majaliwa Bosco  alifariki dunia mara baada ya kung’atwa na nyuki alipokuwa anawarushia mawe juu ya mti chanzo kikiwa ni mchezo wa kitoto.

No comments:

Post a Comment