Thursday, June 13, 2013

Finca yaburutwa CMA Iringa


 

WAFANYAKAZI 13 wa Kampuni ya Finca Tanzania (M.C.F) Ltd Tawi la Irimga waliofukuzwa kazi wanatarajia kuibuza kampuni hiyo katika baraza la Usuluhishi Tawi la Iringa (CMA).

Katibu wa TUICO Mkoa wa Iringa Magasa Chimola aliliambia gazeti hili jana kuwa wafanya kazi hao wlaifika katika ofisi hizo leo na kujaza fomu kwa ajili ya kufungua jarada hilo la kesi.

Kwa uapnde wao wafanya kazi hao walisema hatua ya kufungua shauri katika Tume ya usuluhishi ni kuhakikisha wanapata haki zao ambazo walidai zimekiukwa na kufukuzwa kwao ni kitendo cha uonevu.

Wafanyakazi hao wametaja  sababu za kufukuzwa  kwao  ikiwa ni siku moja tangu  kampuni hiyo kutangaza majina yao kwenye gazeti la Mwananchi  toleo la Julai 13 mwaka huu likiueleza umma kuwa kuanzia sasa watu hao si wafanya kazi wa Kampuni hiyo.

Walitaja sababu  hizo kuwa ni na kitendo chao  cha kuandika barua na kuituma kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni hiyo taifa Mei 16 mwaka huu wakiomba kukutana nae ili kutoa kero zao walizodai zilidumu kwa muda mrefu bila kushughulikiwa na uongozi wa Finca Tawi la Iringa na kanda.

“Kwa mda mrefu tumekuwa tukifanya kazi katika mazingira magumu,tulijaribu kuwasiliana na uongozi wa  tawi  na kanda lakini jitihadi zetu hazikuzaa matunda,na tuliamua kuwasilisha taarifa zetu ngazi za juu na badala ya kutusikiliza madai yetu tulipata barua siku ile ile ya ikitutisha vitisho kutoka kwa Mkurugenzi wetu Taifa”alisema Mmoja wa wafanya kazi hao.

Kero nyiungine walizoziainisha ni pamoja na wafanyakazi kuchelewa kuthibitishw akazini,kucheleweshwa kwa mikopo kwa miezi mingi bila kupewa sababu toka kwa uongozi tawi,wafanyakazi kuwajibika kutoa majibu katika makosa ambayo hawakutenda,kamati ya maadili kuendeshwa kibabe na wafanyakazi kuingia gharama binafsi kufanya kazi za Kampuni.

Wafanya kazi waliotangazw akufukuzwa kazi ni pamoja na Anderw Sharaj, Aneth Shirima,Bony Msindo,Cotrida Mtweve,Damian Msanganzila,Edoxia Mbwilo,Happy Sanga na Mgewa Mbondo.

Wengine ni Mihayo Stepheno,Peter Zephania,Widman Masika ,Hennry Martin na Calvin Mlokozi

 

 

 

No comments:

Post a Comment